Barua pepe: infokvz@.go.tz  |  S.L.P: 2803  |  Simu: +255 779 569 917


Logo
Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo Zanzibar
Logo

HISTORIA YA KVZ

HISTORIA YA KIKOSI CHA VALANTIA

Kikosi cha Valantia Zanzibar kimeanzishwa mwaka 1957 wakati wa harakati za kudai uhuru ambapo vijana wazalendo kwa kushirikiana na chama cha ASP walikuwa miongoni mwao walinzi wa chama hicho.baada ya mapinduzi matukufu miongoni mwa waliojiunga na vikosi vya vya ulinzi na usalama vya SMT na SMZ kama :-

(1)Jeshi la ulinzi la wananchi watanzania (JWTZ).
(2)Usalama wa taifa (TISS).
(3)Polisi.
(4)Kikosi maalumu cha kuzuia magendo(KMKM).

Kipindi chote hicho KVZ ilikuwa inafanya kazi bila malipo na bila sheria hadi mwaka 1982 ikawepo kwa mujibu wa sheria na ikaanzishwa kwa sheria namba 8 ya mwaka 1982 ambapo ilijulikana kwa jina la kikosi maalum cha kujitolea (KMCK).

Ikaendelea hadi mwaka 1992 Tanzania ikaingia katika mfumo wa vyama vingi na kwa kuwa valantia walikuwa katika mfumo wa chama kimoja ,serikali ikaona hakuna haja ya kuwepo kwa valantia.ikaanzishwa rasmi kwa mujibu wa sheria namba 5 ya mwaka 2004.

DIRA

Kikosi cha Valantia kuwa ni chombo muhimu na chenye ufanisi katika kutoa huduma ya Ulinzi wa Nchi, Raia na mali zao pamoja na kuhamasisha ushiriki wa kiulinzi katika Serekali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania

DHAMIRA

Ni kutoa Huduma ya Ulinzi kwa kushirikiana na taasisi nyengine za ulinzi na usalama za Serekali ya Zanzibar na serekali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya kudumisha Amani na mshikamano wa Taifa. KVZ itajitahidi kutekeleza sera ya Taifa hususa sera ya kupunguza umaskini kupitia sera, mipango na majukumu yake ya kila siku ili kuchangia katika kuleta maendeleo ya jamii na Taifa kwa jumla.

Kuanzishwa kwa Kikosi Cha Valantia Zanzibar

Kikosi cha Valantia Zanzibar ni miongoni mwa Idara tano Maalum za Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar kilicho chini ya Afisi ya Rais Tawala za mikoa na Idara Maalum za (SMZ).
Kikosi cha Valantia Kimeanzishwa Kwa Sheria Namba 5 ya Mwaka 2004 na kwa mujibu wa Sheria hiyo kikosi kina majukumu ya kueka amani na utulivu katika nchi, kupambana na janga lolote litakalo ikumba jamii kulinda Viongozi na mali za serekali na kufanya kazi za kijeshi kwa madhumuni ya kuzuia hali inayohatarisha ulinzi na usalama.

Kisiwa cha Unguja
Paris

Ramani ya Kisiwa cha Unguja

Zanzibar ni mkusanyiko wa visiwa vikubwa viwili vya unguja na Pemba, pia vikipakana pembezoni mwake na visiwa vyengine vidogo vidogo kama Changuu. Misali, Pungume na kadhalika.
Zanzibar ni visiwa vinavyopatikana katika bahari ya Hindi, ni visiwa ambavyo vimebarikiwa neema nytingi hususan matunda na nafaka toifauti, pia ina mandahari nzuri kutokana nafukwe zake pamoja na mji wa kihistoria wa mji mkongwe.

Kisiwa cha Pemba
Paris

Ramani ya Kisiwa cha Pemba

Zanzibar ni mkusanyiko wa visiwa vikubwa viwili vya unguja na Pemba, pia vikipakana pembezoni mwake na visiwa vyengine vidogo vidogo kama Changuu. Misali, Pungume na kadhalika.
Zanzibar ni visiwa vinavyopatikana katika bahari ya Hindi, ni visiwa ambavyo vimebarikiwa neema nytingi hususan matunda na nafaka toifauti, pia ina mandahari nzuri kutokana nafukwe zake pamoja na mji wa kihistoria wa mji mkongwe.


Picha za Maafisa waliowahi kuwa wakuu wa KVZ

historia2
LT COL : Said A Juma Shamhuna

Mkuu wa Kikosi Cha Valantia Zanzibar
(2019 - today)

Wasifu
historia2
Lt COL : MM KOMBO

Mkuu wa Kikosi Cha Valantia Zanzibar
(2013 - 2019)

wasifu
historia2
COL : NW MAGETA

Mkuu wa Kikosi Cha Valantia Zanzibar
(2008 - 2011)

wasifu

historia2
COL : I A ABDULRAHMAN

Mkuu wa Kikosi Cha Valantia Zanzibar
(2002 - 2006)

wasifu

© 2021 Kikosi Cha Valantia Zanzibar. Haki zote zimehifadhiwa