Barua pepe: infokvz@.go.tz  |  S.L.P: 2803  |  Simu: +255 779 569 917


Logo
Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo Zanzibar
Logo

SANAA NA MICHEZO KVZ

MPIRA WA MIGUU - KVZ
Car
TIMU YA MPIRA WA MIGUU KIKOSI CHA VALANTIA ZANZIBAR

Kvz Fc ilianzishwa 20/07/2004 kwa wakati huo inajulikana kwa jina la kvz sport club, timu hiyo ilianzishwa chuo cha pangatupu. Tulianza kuingia kwenye ligi daraja la tatu Mahonda katika wilaya ya kaskazini (B) Mkoa wa kaskazini Unguja kuanzia msimu wa mwaka 2004-2005 na tumepanda daraja la pili wilaya.

Tulishinda ligi hiyo ya daraya la pili kwa muda wa miaka mine (4) kuanzia 2005-2009 tukapanda daraja la kwanza kanda kabla ya kuanza kupanda kanda ZFA ilibadilisha mfumo mwingine wa ligi badala ya kucheza kanda ilikuwa ligi daraja la pili taifa ili kuwa ni mwaka 2010. Kutoka 2010-2011 tukaingia rasmin kucheza daraja la kwanza kanda kutoka 2011-2014 timu yetu ilipanda na kucheza ligi kuu ya Zanzibar (Primer league) tumeanza kucheza ligi kuu mwaka 2015 hadi leo. Mnamo mwaka 2017 tukawa mabingwa FA Cup. Ambapo tulishiriki kombe la shirikisho barani Afrika na kusafiri hadi Burundi kucheza na timu ya Masenger Ngozi FC. Pia ndio mwaka huo ndio tumebadilisha jina na kuitwa KVZ Fc, badala ya KVZ sport club ilipofika mwaka 2019-2020 KVZ Fc ilipata ubingwa tena wa FA cup na kushiriki kombe la shirikisho kwa mara pilina kwenda kucheza huko Sudan na timu ya AL-ETBARA.

MPIRA WA MIKONO KIKOSI CHA VALANTIA ZANZIBAR
Car
TIMU YA MPIRA WA MIKONO WANAWAKE KIKOSI CHA VALANTIA ZANZIBAR

Mchezo huo ulianzishwa mwishoni mwa karne ya 19 kaskazini mwa Ulaya na Ujerumani. Sheria ya kisasa ya mchezo ilichapishwa mnamo mwaka wa 1917 nchini Ujerumani, na ilikuwa na marekebisho kadhaa tangu hapo.

Mechi za kwanza za kimataifa zilichezwa chini ya sheria hizi kwa wanaume mwaka wa 1925 na kwa wanawake mwaka wa 1930. Mpira wa mkono wa wanaume ulichezwa mara ya kwanza katika michezo ya Olimpiki ya majira ya joto ya 1936 huko Berlin kama nje, na wakati ujao katika michezo ya Olimpiki ya majira ya joto ya 1972 huko Munich kama ndani, na umekuwa mchezo wa Olimpiki tangu hapo. Kwa timu ya wanawake uliongezwa katika michezo ya Olimpiki ya majira ya joto ya 1976.

Shirika la Kimataifa la Mpira wa mkono lilianzishwa mwaka wa 1946 na kufikia mwaka wa 2016 limekuwa na mashirika ya wanachama 197. Mchezo huu unajulikana sana katika nchi za bara la Ulaya, ambazo zilishinda medali zote ila moja katika michuano ya dunia ya wanaume tangu 1938. Katika michuano ya dunia ya wanawake, nchi mbili tu zisizo za Ulaya zimeshinda jina: Korea Kusini na Brazil. Mchezo pia unapata umaarufu katika Mashariki ya Mbali, Afrika Kaskazini na sehemu za Amerika ya Kusini.

UTAMADUNI/MAIGIZO - KVZ
Car
UTAMADUNI NA MAGIZO NI NJIA MOJA WAPO YA KUTANGAZA TAIFA LETU

Sanaa hujumuisha

Muziki

Ambao unaweza kuwa wa kuimba na wa vyombo uliorekodiwa kwa sauti au utunzi wa muziki ulioandikwa, bendi, muziki wa jazi, ala, uliorekodiwa, video, taarabu, kwaya, gwaride,muziki wa asili wa ngoma na unaoambatana na maigizo na thamthiliya.

Sanaa za Ufundi

Hujumuisha picha za kuchorwa kwa rangi, uchoraji wa kawaida, michoro ya majalada, vitabu au magazeti, uchoraji wa kwenye vitu vigumu kama metali au mbao, uandishi wa herufi ulionakishiwa, sanaa za vikaragosi kwa kutumia kompyuta na michoro iliyochapishwa. Ramani, michoro ya majengo na vielelezo, sanaa za kuumba na kuchonga, picha mgando za kamera, Kazi za usanifu majengo katika maumbo Sanaa za viwandani ikiwa pamoja na zilizo katika picha au zilizofumwa na urembo, na ubunifu wa mavazi, ususi na useketaji wa nguo.

Sanaa za Maonyesho

Michezo ya kuigiza ya jukwaani, maigizo bubu, usanifu wa majukwaa, maleba, mapambo, uandishi wa tamthiliya, ngoma na ubunifu wake, sauti na vifaa vya jukwaani, sarakasi za binadamu au za wanyama, michezo ya redio..

Car
TARAARABU KIKOSI CHA VALANTIA ZANZIBAR

Sanaa hujumuisha

Muziki

Ambao unaweza kuwa wa kuimba na wa vyombo uliorekodiwa kwa sauti au utunzi wa muziki ulioandikwa, bendi, muziki wa jazi, ala, uliorekodiwa, video, taarabu, kwaya, gwaride,muziki wa asili wa ngoma na unaoambatana na maigizo na thamthiliya.

Sanaa za Ufundi

Hujumuisha picha za kuchorwa kwa rangi, uchoraji wa kawaida, michoro ya majalada, vitabu au magazeti, uchoraji wa kwenye vitu vigumu kama metali au mbao, uandishi wa herufi ulionakishiwa, sanaa za vikaragosi kwa kutumia kompyuta na michoro iliyochapishwa. Ramani, michoro ya majengo na vielelezo, sanaa za kuumba na kuchonga, picha mgando za kamera, Kazi za usanifu majengo katika maumbo Sanaa za viwandani ikiwa pamoja na zilizo katika picha au zilizofumwa na urembo, na ubunifu wa mavazi, ususi na useketaji wa nguo.

Sanaa za Maonyesho

Michezo ya kuigiza ya jukwaani, maigizo bubu, usanifu wa majukwaa, maleba, mapambo, uandishi wa tamthiliya, ngoma na ubunifu wake, sauti na vifaa vya jukwaani, sarakasi za binadamu au za wanyama, michezo ya redio..

Car
KIKUNDI CHA MAZOEZI KVZ MTONI

mazoezi

Chimbuko la mazoezi katika kikosi cha Valantia Zanzibar

Kikundi cha mazoezi katika kikosi cha valantia zanzibar kilianzishwa mnamo mwaka 2018 chini ya kamanda mkuu wa kikosi hiko Lt col MM Kombo ambapo ndio muasisi mkuu wa kikundi hiko hapo kikosini .

mazoezi ni afya

.

Sanaa za Maonyesho

Michezo ya kuigiza ya jukwaani, maigizo bubu, usanifu wa majukwaa, maleba, mapambo, uandishi wa tamthiliya, ngoma na ubunifu wake, sauti na vifaa vya jukwaani, sarakasi za binadamu au za wanyama, michezo ya redio..


© 2021 Kikosi Cha Valantia Zanzibar. Haki zote zimehifadhiwa